Karibu Musoma Information Center kwa huduma zifuatazo:- 1) Kwa kutengenezewa design mbalimbali kama za Business card, Vipeperushi, mabango mbalimbali, kadi za Harusi za kisasa zaidi, kadi za mialiko mbalimbali, Vitambulisho vya wanafunzi wa sekondari na katika kampuni mbalimbali ( ID cards) na kadi nyinginezo zenye design ya kuvutia. 2) Kutengenezewa mabango ( Posters) mbalimbali zinazohusu biashara ya mhusika au bidhaa mbalimbali. 3) Kutengenezewa nembo ( LOGO) za kuhusiana kampuni au biashara yako. 4) Tunatengeneza tovuti ( Websites ) zenye kiwango ambacho huwezi amini kama zinatengenezwa musoma, kwa bei nafuu ambayo huwezi ipata kwingine isipo kuwa kwetu. 5) Mwisho tunatoa ushauri na elimu kuhusiana na maswala ya computer.5) Sisi ni watengenezaji wa blog zinazokaa mfumo wa website. kama hii unayoiona.
Home » » KWA PAMOJA TUTAFANIKIWA TUNAOMBA MSAADA WAKO.

KWA PAMOJA TUTAFANIKIWA TUNAOMBA MSAADA WAKO.





Taasisi ya kuhamasisha maendeleo na mawasiliano katika jamii yenye makao yake mjini Musoma mkoani Mara ya JAMII INFORMATION NETWORK inatarajia kufanya Kongamano kubwa litakalo wahusisha  Wanafunzi zaidi ya 200 kutoka Shule 10 za Sekondari za Manispaa ya Musoma Mwezi August Mwaka huu, ikiwa ni njia ya kuhamasisha Maendeleo na kuimarishaji wa Mawasiliano ndani ya Jamii.

Katika Kongamano hilo mada mbalimbali zitatolewa na Wataalamu waliobobea katika Masuala uhamasishaji wa Vijana Kupambana dhidi ya Ukimwi,ujasiriamali,dhana ya kujiajiri,Changamoto katika Elimu kwa Vijana  pamoja na Ukatili wa Kijinsia ikiwa ni njia ya kujenga Msingi bora wa Makuzi kwa Vijana wetu.

Mbali na hivyo vijana hao pia wataelezwa jinsi ya kuwa Wazalendo katika nchi yao,kupambana na rushwa,Umaskini lakini pia wakipata elimu sahihi ya faida za uwekezaji kwa Tanzania,Sababu za Mimba za Mapema kwa watoto wa kike na jinsi ya kujenga Mahusiano na Mawasiliano yaliyo sahihi.

Pamoja na Mtandao huu kuwa na nia njema katika kuwasaidia Vijana lakini bado kumekuwepo na Changamoto mbalimbali katika kufanikisha Kongamano hilo hasa katika Suala la kifedha,hivyo basi Taasisi ya JAMII INFORMATION NETWORK kwa nia njema inakuomba wewe Mtanzania,Mpenda Maendeleo,unaekaa ndani au nje ya nchi,Mashirika kusaidia Taasisi hii katika kufanikisha Kongamano hilo ili vijana wetu wakue katika Makuzi mema na kujenga Tanzania ya kesho  iliyostaarabika.

 Blog Master
Like us on Facebook
Follow us on Twitter
Recommend us on Google Plus
Subscribe me on RSS