Karibu Musoma Information Center kwa huduma zifuatazo:- 1) Kwa kutengenezewa design mbalimbali kama za Business card, Vipeperushi, mabango mbalimbali, kadi za Harusi za kisasa zaidi, kadi za mialiko mbalimbali, Vitambulisho vya wanafunzi wa sekondari na katika kampuni mbalimbali ( ID cards) na kadi nyinginezo zenye design ya kuvutia. 2) Kutengenezewa mabango ( Posters) mbalimbali zinazohusu biashara ya mhusika au bidhaa mbalimbali. 3) Kutengenezewa nembo ( LOGO) za kuhusiana kampuni au biashara yako. 4) Tunatengeneza tovuti ( Websites ) zenye kiwango ambacho huwezi amini kama zinatengenezwa musoma, kwa bei nafuu ambayo huwezi ipata kwingine isipo kuwa kwetu. 5) Mwisho tunatoa ushauri na elimu kuhusiana na maswala ya computer.5) Sisi ni watengenezaji wa blog zinazokaa mfumo wa website. kama hii unayoiona.

Discover JIN

Asasi hii ilianzishwa hapa Musoma kuanzia mwezi Februari mwaka 2011 ikiwa na wanachama waasisi kumi (10). Wazo la kuanzisha Asasi hii lilitokana na ukweli kwamba moja ya vikwazo vinavyosababisha kudorora kwa maendeleo katika jamii za nchi zinazoendelea ni kukosekana kwa taarifa sahihi na za wakati. Asilimia kubwa ya jamii ya Watanzania wanaishi nje ya miji ambako kuna uhaba wa vyombo vya kupashana habari kama vile magazeti, radio, luninga, internet n.k. Kukosekana kwa taarifa za mambo yanayofanyika ndani ya jamii na nje ya jamii waliyomo kunawanyima fursa ya kushiriki katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni ili kwenda na mabadiliko katika dunia ya leo ya sayansi, tekinolojia na utandawazi.
DIRA
Kuwa na jamii yenye uelewa mpana wa habari sahihi za masuala ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni na kutambua mabadiliko yanayotokea kati yake na jamii zingine ili kukabiliana na changamoto za kimaendeleo.
DHAMIRA
Asasi inadhamiria kushiriki na kushirikisha ngazi zote za kijamii hasa makundi yaliyoko pembezoni katika ukusanyaji, uandikaji, usambazaji na upashanaji habari.
MADHUMUNI
Kuhabarisha jamii jinsi ya kukabiliana na changamoto za athari na madhara umasikini,
Rushwa na VVU/UKIMWI.
Kushirikisha jamii katika ukusanyaji wa taarifa muhimu, kuziandika na kuzisambaza ili
Kuimarisha mawasiliano ya habari.
Kuimarisha mitandao ya mawasiliano ndani ya jamii ili jamii iweze kupata taarifa sahihi
Zinazoendana na wakati.
Kushirikisha jamii katika kuibua changamoto na kukuza ushawishi na utetezi wa sera
Mbalimbali kwa njia ya midaharo ili ziwe na tija kwa jamii.
Kufanya tafiti mbalimbali za masuala ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni ili kuzipatia
Ufumbuzi.
Kuyajengea uwezo makundi mbalimbali ya kijamii Kwa njia ya vipeperushi, magazeti,
Radio, TV na mafunzo ili kupata ufahamu wa kujiletea mabadiliko.
Kukuza uelewa wa jamii juu ya kutambua na kutetea haki zao za msingi zinazokiuka Misingi ya demokrasia, usawa, utawala bora, uwazi na uwajibikaji.
Like us on Facebook
Follow us on Twitter
Recommend us on Google Plus
Subscribe me on RSS