UKATILI WA AINA HUU LAZIMA TUUPINGE KWA NGUVU ZOTE
Posted by jamii information network
Posted on Tuesday, April 23, 2013
VIJANA WA SHULE ZA SEKONDARI ZAIDI YA 200 KUPEWA ELIMU MBADALA MKOANI MARA KUPITIA JAMII INFORMATION NETWORK (JIN)
Posted by jamii information network
Posted on Monday, April 22, 2013
HABARI KATIKA PICHA
Posted by jamii information network
Posted on Sunday, January 20, 2013
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Matongo wakiangalia bwawa la Maji
Baadhi ya wataalamu kutoka Mgodi wa North Mara wakifafanua Jambo kwa Waandishi wa Habari
KUHUSU JAMII INFORMATION NETWORK (JIN)
Posted by jamii information network
Posted on Sunday, January 13, 2013
Asasi hii ilianzishwa hapa Musoma kuanzia mwezi Februari mwaka 2011 ikiwa
na wanachama waasisi kumi (10). Wazo la kuanzisha Asasi hii lilitokana na
ukweli kwamba moja ya vikwazo vinavyosababisha kudorora kwa maendeleo katika
jamii za nchi zinazoendelea ni kukosekana kwa taarifa sahihi na za wakati.
Asilimia kubwa ya jamii ya Watanzania wanaishi nje ya miji ambako kuna uhaba wa
vyombo vya kupashana habari kama vile magazeti, radio, luninga, internet n.k.
Kukosekana kwa taarifa za mambo yanayofanyika ndani ya jamii na nje ya jamii
waliyomo kunawanyima fursa ya kushiriki katika kukabiliana na changamoto
mbalimbali za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni ili kwenda na mabadiliko katika
dunia ya leo ya sayansi, tekinolojia na utandawazi.
DIRA
Kuwa na jamii yenye uelewa mpana wa habari sahihi za masuala ya
kijamii, kiuchumi na kiutamaduni na kutambua mabadiliko yanayotokea kati yake
na jamii zingine ili kukabiliana na changamoto za kimaendeleo.
DHAMIRA
Asasi inadhamiria kushiriki na kushirikisha ngazi zote za kijamii hasa
makundi yaliyoko pembezoni katika ukusanyaji, uandikaji, usambazaji na
upashanaji habari.
MADHUMUNI
Kuhabarisha jamii jinsi ya
kukabiliana na changamoto za athari na madhara umasikini,
Rushwa na VVU/UKIMWI.
Kushirikisha jamii katika
ukusanyaji wa taarifa muhimu, kuziandika na kuzisambaza ili
Kuimarisha mawasiliano ya
habari.
Kuimarisha mitandao ya mawasiliano ndani ya jamii ili jamii iweze
kupata taarifa sahihi
Zinazoendana na wakati.
Kushirikisha jamii katika kuibua
changamoto na kukuza ushawishi na utetezi wa sera
Mbalimbali kwa njia ya midaharo ili
ziwe na tija kwa jamii.
Kufanya tafiti mbalimbali za masuala ya
kijamii, kiuchumi na kiutamaduni ili kuzipatia
Ufumbuzi.
Kuyajengea uwezo makundi mbalimbali ya kijamii Kwa njia ya vipeperushi,
magazeti,
Radio, TV na mafunzo ili kupata
ufahamu wa kujiletea mabadiliko.
Kukuza uelewa wa jamii juu ya kutambua na kutetea haki zao za msingi
zinazokiuka Misingi ya demokrasia,
usawa, utawala bora, uwazi na uwajibikaji.
JAMII YENYE UPENDO UFANIKIWA KWA KILA JAMBO
Posted by jamii information network
Posted on Saturday, January 12, 2013
VIJANA 200 KUJITAMBUA MKOANI MARA
Posted by jamii information network
Posted on Saturday, January 05, 2013
ZAIDI YA VIJANA 200 KUJITAMBUA MKOANI MARA
Taasisi isiyo ya Kiserikali
inayojishughulisha ya utoaji elimu katka
Masuala mbalimbali katika Jamii,kuibua changamoto na kusaidia Makundi
yasiyojiweza ya Jamii Information Network (JIN)
inatarajia kuendesha kongamano la
vijana mjini hapa mwaka huu wa 2013.
Akiongea na waandishi wa habari
ofisini kwake Mjini Musoma,Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Augustine Mgendi amesema
Kongamano hilo linatarajia kufanyika huku likiwakutanisha Vijana zaidi ya 200 kutoka
Shule 10 za Mjini hapa ambapo linalenga kuwajengea stadi za kujitambua,kujiamini
na kujithamini.
Alisema katika Kongamano hilo vijana hao watafundishwa kukabiliana na
changamoto zinazowakabili katika makuzi yao lakini pia kuhamasisha Vijana kupambana na Ugonjwa
wa Ukimwi,kujifunza mbinu za Ujasirimali,dhana ya kujiajiri na Changamoto
zake vijana kujenga Uzalendo,kupambana na Umaskini,Rushwa ,Kuepuka Mimba za Utotoni katika
Jamii.
‘Nadhani Vijana bado wanachangamoto kubwa sana katika kufanikisha ndoto
zao na hii ni fursa pekee kwa Vijana kujifunza Mbinu mbalimbali maana tutakuwa
na wataalam ambao wamebobea katika mambo hayo ili kutoa Mwanga kwa Vijana wetu
” alisema Mkurugenzi huyo
Mkurugenzi huyo alisema kuwa Shule
zitakazoshiriki Kongamano hilo zitatajwa baadaye baada ya Mambo kadha wa kadha
kukamilika
“Ni Shule kumi zitakazoshiriki na mambo yakiwa tayari tutawafahamisaha
ni shule gani ambazo tutakuwa nazo” alisema Mkurugenzi huyo
Mkurugenzi huyo alisema kuwa watakuwepo
wataalamu mbalimbali watakaohusika kutoa mafunzo katika Kongamano hilo huku
akisema kuwa Vijana ndiyo nguvu kubwa ya
Taifa kwasasa hivyo wanahitaj miongozo ya Kimaisha katika kujitambua.
Kongamano hilo ambalo litakuwa linafanyika
kila Mwaka litakuwa na kauli mbiu mbalimbali ambapo alisema kwa Mwaka huu litakuwa na Kauli mbiu
ya “Jitambue Kijana” ambapo alisema kuwa
Kongamano hilo litawasaidia Vijana
wengi Kujitambua kutokana na Changamoto
zinazowakabili kwasasa.
“Tunatarajia
Kongamano hili liwe linafanyika kila Mwaka ili kutoa elimu
na mwongozo wa kimaisha kwa vijana na
kwa kuanza mwaka huu kauli mbiu yetu itafahamika kama Jitambue Kijana
hii ni kutokana na vijana wengi kutofikia Malengo yako kutona na
Changamoto
zilizopo”alisema Bw Mgendi
Mbali na Kongamano hilo taasisi ya
Jamii Information Network ambayo hufanya
shughuli zake mkoa wa Mara inatarajia kutoa elimu mbalimba mkoani Mara ili
jamii huska kwenda na wakati kutokana asilimia kubwa ya Watanzania kuishi
vijijini ambapo vyombo vya habari kufika inakuwa tabu.
Aidha Mkurugenzi huyo alisema
kuwa Taasisi hiyo inatarajia kutumia
wanahabari mkoani Mara kuibua changamoto mbalimbali zilizopo vijijini ili
kuziweka bayana na kufanya vipindi mbalimbali kutoka Vijijini ambavyo alisema
vitaibua Changamoto zilizopo huko.
Katika kufanikisha Kongamano hilo
Mkurugenzi huyo ameyaomba Mashirika mbalimbali kujitokeza kufadhili
Kongamano hilo ambalo litakuwa ni msaada mkubwa wa kuwajenga Vijana hasa mkoani Mara.
“Mimi nayaomba mashirika mbalimbali kujitokeza
ili kufanikisha Kongamano hilo maana najua litakuwa msaada mkubwa sana kwa
Vijana ambapo kwa njia moja au nyingne
litaweza kubadili fikra za vijana wanapomaliza masomo yao’ alimalizia
Mkurugenzi huyo
Nguvu kazi ya taifa lolote duniani
ni vijana,hivyo wasipoandaliwa vizuri leo,kesho watakuwa bomu ambalo
litakapolipuka litaangamiza taifa lote.Waafrika wanayo methali isemayo “mtoto
umleavyo ndivyo akuavyo”,hivyo kama tunahitaji kuwa na kizazi bora chenye
maadili,uzalendo na uwajibikaji tuanze kuwaandaa vijana sasa
kisaikolojia,kimaadili na kimtazamo
Afisa Habari na Uhamasishaji
Jamii Information Network
MAZISHI YA SAJUKI YALIVYOKUWA
Posted by jamii information network
Posted on Friday, January 04, 2013
HIVI NDIVYO MAZISHI YA MPENDWA WETU SAJUKI YALIVYOKUWA - RAISI AUDHURIA
![]() |
| Mwili wa marehemu Sajuki ukipelekwa makaburini. |
![]() | |
Maiti ambayo bado haijafahamika
Posted by jamii information network
Posted on Friday, January 04, 2013
MAITI YA MTU AMBAYE HAKUWEZA KUFAHAMIKA IMEKUTWA IMEFUKIWA KWA MAWE NA UDONGO HUKO MAKOKO KATIKA MANISPAA YA MUSOMA
| KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOANI MARA ABSALOM MWAKYOMA AKIWA NA MWANA HABARI GEORGE MARATO |
Na Shomari Binda
Musoma,
Maiti ya mtu mmoja ambaye hakuweza kufahamika imekutwa imefukiwa kandokando ya miamba ya milima kwa mawe na udongo katika mtaa wa Nyarigamba Kata ya Makoko Manispaa ya Musoma na kuendelea kuwa na hofu kwa Wananchi juu ya mauaji yanayoendelea kutokea katika maeneo mbalimbali katika siku za hivi karibuni.
Katika taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi Mkoani Mara ilisema awali kulikuwepo na uvumi uliohusisha mwili wa marehemu na mwanamke mmoja ambaye amepotea na hajulikani alipo toka tarehe 14.12.2012 katika mazingira ya utatanishi anayeishi katika mtaa wa Ziwani katika kata hiyo ya Makoko.
Taarifa hiyo ilisema baada ya Mwili huo kufanyiwa uchunguzi na madaktari katika hospitali ya Mkoa wa Mara imebainika kuwa mwili huo uliokuwa umefukiwa haujulikani ni wa nani huku ndugu wa Mwanamke aliyepotea wamethibitisha mwili huo sio wa ndugu yao.
"Natoa wito kwa Wananchi wa Musoma na vitongoji vyake pamoja na sehemu nyingine wafike katika Hospitali ya Mkoa wa Mara katika chumba cha kuhifadhia maiti ili kujaribu kuutambua mwili huo ambao umehifadhiwa pale,"alisema Kamanda Mwakyoma.
Mmoja wa shuhuda wa tukio la kufukuliwa kwa mtu huyo Vedastus Masige aliyezungumza na bLOG HII alisema Jeshi la Polisi bado halijaweka nia ya dhati ya kukabiliana na matukio hayo licha kulipotiwa na vyombo vya Habari lakini wamekuwa wakipuuzia huku Wananchi wakiendelea kuangamia.
Alisema hawajasikia Jeshi la Polisi limefikia wapi katika kuchukua hatua juu ya kukabiliana na hali hiyo huku mauaji yakiendelea kutokea na kuwafanya Wananchi wakiishi kwa mashaka na wasiwasi kutokana na hali hiyo inavyoendelea kutokea.
''Tulishuhudia katika siku za nyuma Jeshi la Polisi likihamia Wilayani Serengeti likiongozwa na Kamanda wa Oparesheni wa Jeshi la Polisi Tanzania Chagonja kutokana na kifo cha Mtalii mmoja na waliohusika kukamatwa leo kwa nini wanashindwa kupambana na mauaji yanayokuwa yanatokea mara kwa mara Musoma na Mkoa wa Mara kwa ujumla.
"Haiwezekani kwenye Nchi yetu tuishi kama wakimbizi matukio ya mauaji ya ajabu yamekuwa yakitokea rakini hatua za haraka zimekuwa hazichukuliwi hali ambayo inaendelea kutupa hofu na kuishi kwa mashaka tukiwa katika ardhi yetu inayodaiwa kuwa ni kisima cha Amani,''alisema Vedastus.
Taarifa za kupatikana kwa mwili huo zilitolewa na wavuvi wa dagaa waliokuwa wakianika kwenye jiwe maeneo ya Makoko nje kidogo ya Mji wa Musoma na kusikia harufu ambayo iliwashitua na kuanza kuulizana ni harufu ya kitu gani na inatokea wapi.
"Siku ya kwanza tulisikia harufu lakini tulichukulia ni kawaida lakini muda ulivyozidi kwenda tuliona ikiendelea kuongezeka na kuamua kufatilia kwa kushirikiana na baadhi ya askari wa Jeshi la Wananchi ambao tunaishi nao jirani na kubaini kuna kitu kimefukiwa pembeni ya mlima na kuamua kulitaarifu Jeshi la Polisi,"alisema mmoja wa wavuvi hao aliyekuwa katika eneo la tukio.








